Rasmi Tanasha Apata Mrithi wa Diamond
BAADA ya kuachana na staa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, maisha ya Tanasha Donna ya kimapenzi hayajakuwa kwenye mitandao ya kijamii.
Lakini kwa sasa ni rasmi kwamba Tanasha amepata mrithi wa jamaa huyo baada ya kuvunja ukimya kwa mmoja wa mashabiki wake aliyemuuliza kama ana mpenzi ambapo alikuwa na haya ya kumjibu;“Nina umakini zaidi kuzingatia kazi yangu, lakini nina mtu ambaye yuko kwa akili yangu, polepole anaingia kwenye moyo wangu.”Pia ameweka wazi kwamba katika maisha yake hajawahi kuolewa.