The House of Favourite Newspapers

RC Makonda Atembelea Ofisi za Clouds Media Group Kutoa Pole

0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,  Paul Makonda (wa pili kulia),  akinena jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga (kushoto).

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Paul Makonda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Dar es Salaam mapema leo ametembelea Ofisi za Clouds Media Group kutoa pole ikiwa ni siku moja baada ya ofisi hizo kukumbwa na janga la moto uliotokea hapo jana majira ya saa nne asubuhi.

Makonda akiongea na maofisa wa vikosi vya usalama.

 

Viongozi wengine wa serikali waliofika ofisini hapo ni Mkuu wa Wilaya wa Kinondoni, Ally Hapi na Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta.

 

Hata hivyo, tayari matangazo ya vituo vya Clouds FM na Clouds TV yamerejea hewani baada ya kupotea siku nzima  jana kutokana na hitilafu ya iliyosababishwa na moto huo ambao chanzo chake hadi sasa hakijajulikana.

JENGO LA CLOUDS MEDIA GROUP LAUNGUA MOTO (Pichaz + Video)

Leave A Reply