Katika hatua nyingine RC Makonda amemtaka mwenyekiti wa wa Mtaa huo wa Msigani Israel Mushi kutofanya kazi kwa upendeleo kwani kuna Mkazi aliyefahamika kwa jina la Maureen Gomba ambaye amelalamikia kuwa mwenyekiti huyo amekuwa akigawa vizimba kwa watu anaowafahamu.
RC Makonda amewatoa hofu wakazi hao kuhusu huduma ya maji na kwani kwasasa mradi huo upo chini ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka DAWASCO, huku Mkuu wa Wilaya hiyo akihaidi kukutana na wananchi hao ili kumaliza kero hiyo kabisa ifikapo Desemba 21.
Comments are closed.