The House of Favourite Newspapers

Safari za Rais Biden za Australia na Papua New Guinea Zimeahirishwa

0
Rais wa Marekani Joe Biden

Rais wa Marekani Joe Biden, Spika wa Baraza la Wawakilishi Kevin McCarthy, na viongozi wengine wakuu wa bunge walionekana kutofikia makubaliano Jumanne, ya kuongeza kiwango cha deni la taifa.

Hali hiyo imejiri huku wizara ya fedha ya Marekani ikioonya kwamba kutokuwepo kwa makubaliano kunaweza kusababisha hofu duniani na janga, wakati rais Biden anajiandaa kuondoka Jumatano kwa mkutano mkuu nchini Japan na nchi saba tajiri zaidi duniani, G7.

Mgogoro huo umeathiri mipango ya Biden ya kutembelea Papua New Guinea na Australia baada ya mkutano huo, White House ilisema katika taarifa.

Mratibu wa baraza la usalama wa taifa wa mawasiliano ya kimkakati John Kirby, aliwaambia wanahabari Jumanne kwamba rais Biden, atakwenda Hiroshima, Japan, leo kama ilivyopangwa kuhudhuria mkutano huo wa mkutano wa G7.

Kutoka Japan, rais Biden alikuwa amepangiwa kwenda Sydney, kwa mkutano wa Quad na kusimama kwa muda mfupi Port Moresby, Papua New Guinea, kukutana na viongozi wa mkutano wa visiwa vya Pasifiki.

Safari hizo sasa zimefutwa, kulingana na Ikulu ya Marekani.

UCHAMBUZI wa SHAFII DAUDA KUELEKEA MECHI ya YANGA na MARUMO GALLANTS – “MARUMO HAWANA cha KUPOTEZA”

Leave A Reply