The House of Favourite Newspapers

Samatta, Kessy Kuifuata Stars Burundi

BADO haijajulikana Mbwana Samatta atatua muda gani kwenye kikosi cha Taifa Stars lakini Farid Mussa na Himid Mao wameshawasili na wanapiga mzigo.

 

Simon Msuva na Hassan Kessy wanajiunga Stars moja kwa moja nchini Burundi tayari kwa mechi ya Jumatano kwenye Uwanja wa Prince Louis Rwagasore kuwania kufuzu Kombe la Dunia.

Akizungumza na Spoti Xtra, Meneja wa Stars, Danny Msangi, amesema; “Samatta yeye bado haijajulikana kama atajiunga na timu hapa Dar au ataunganisha Burundi kwa kuwa timu yake ina mechi Jumapili (leo) hivyo akimaliza majukumu hayo ndiyo itajulikana atajiunga na timu wapi.”

 

“Timu itaondoka Jumanne asubuhi na Ndege ya ATC,” alisema Msangi

KHADIJA MNGWAI, Dar

Comments are closed.