CHAMA cha wasindikaji wa vyakula nchini (Tanzania Food Processors Association – TAFOPA) kinatarajiwa kufanya mkutano wake wa wadau wa uwekezaji wa viwanda vya usindikaji wa vyakula utakaofunguliwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu, Desemba 3 mwaka huu.
Kutoka kushoto ni Mtaalam Mshauri wa TAFOPA, Gloria Kavishe, Mwenyekiti Suzzy Laiser na Makamu Mwenyekiti wa TAFOPA, Janet Mkony.
Mwenyekiti wa TAFOPA, Suzzy Laiser, amesema hayo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na wanahabari kwamba mkutano huo utaleta pamoja zaidi ya wadau 100 wakiwemo mawaziri na wakurugenzi wa idara mbalimbali za serikali na taasisi binafsi.
Baadhi ya wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Amesema lengo la mkutano huo ni kuzindua uanzishwaji na uendelezaji wa maeneo ya viwanda vya usindikaji ili kuhamasisha na kutafuta washirika kutoka mashirika ya kimataifa ambapo pia watajadili mambo mbalimbali yakiwemo kuunda timu ya wataalamu wa kukusanya takwimu na kuandaa andiko la mpango wa kutafuta raslimali.
Na Denis Mtima/GPL
Comments are closed.