Serikali Yamfungia Roma Kisa ‘KIBAMIA’
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza amemfungia Rapa Ibrahim Mussa ‘Roma Mkatoliki’ kwa muda wa miezi sita kutojihusisha na sanaa ya muziki kutokana na kutotii agizo la Wizara hiyo lililomtaka kubadilisha maudhui ya wimbo wake wa KIBAMIA.
Kutokana na wimbo huo ambao Roma amewashirikisha wasanii wenzake, Stamina na Maua Sama, Basata walimuita na kumweleza arekebishe maudhui ya wimbo lakini inasemekana hakutekeleza agizo.
Comments are closed.