Shigongo Aishauri Serikali Juu ya Lugha Maalum ya Kufundishia
MBUNGE wa Jimbo la Buchosa kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Eric Shigongo amehoji juu ya msimamo wa Serikali kuhusu Lugha ya kufundishia kwa ngazi ya Elimu zote kuanzia shule ya msingi.
Shigongo amehoji suala hilo kwenye kikao Bungeni leo ambapo amebainisha kuwa Nchi lazima iwe na Lugha ya kufundishia ambayo itawasaidia wanafunzi kuweza kuelewa na kutofeli kwa sababu ya changamoto ya lugha.