Mgombea Ubunge kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM),Eric Shigong James jana amefika nyumbani kwa familia ya Nyaga Mirambo kuifariji kutokana na kuondokewa na mpendwa wao, Ntumbi Manyaga ambaye ni baba wa familia hiyo aliyefariki dunia Septemba 16 mwaka huu. Akiwa msibani hapo aliweza kuungana na ndugu, jamaa na marafiki katika kuwapa pole kutokana na msiba huo.