The House of Favourite Newspapers

Shoo ya Kanye West yakumbwa na ghasia New York

0

kanye-west-adidas-yeezy-boost-350-jumping-1

Shoo ya ghafla iliyofanywa na rapa wa Marekani, Kanye West mjini New York, iliahirishwa baada ya maelfu ya mashabiki kufika eneo la shoo na kuzua ghasia.

Zaidi ya mashabiki 4000 walifika katika ukumbi wa Webster ulio na uwezo wa kuchukua watu 1500.

Mashabiki walimiminika barabarani na kisha kupanda juu ya magari wakichungulia kupitia madirisha, angalu kumuona mwanamuziki huyo.

Kanye alisema kuwa atafanya shoo hiyo ya ghafla kwenye mitandao ya kijamii baada ile ya mji wa New York kufutwa kutokana na hali mbaya ya hewa.

Leave A Reply