SIKUKUU YA EID EL FITR ILIVYOFANA COCO BEACH, DAR
Sehemu ya wakazi wa maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam wakiwa kwenye ufukwe wa Coco Beach jioni ya leo ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Sikukuu ya Eid El Fitr.
Mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na maeneo ya jirani leo walifurika kwa wingi katika Ufukwe wa Coco Beach ikiwa ni sehemu ya kusherehekea sikukuu ya Idd Pili duniani kwa waumini wa Kiislam.
Sikukuu ya Idd hufanyika kila mwaka duniani baada ya Waislam kumaliza mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaowataka waumini hao pamoja na kutokula mchana, kujiimarisha katika kutenda mambo mema kwa binadamu wenzao na hivyo kwa Mwenyezi Mungu.
Comments are closed.