The House of Favourite Newspapers

Simba kumfuata Mavugo Ufaransa

0

mavugo-agiye-kugaruka-muri-kiyovu-_53f3764f70777Straika Laudit Mavugo.

Na Khadija Mngwai, Dar es Salaam – Championi Jumamosi

KIROHO safi Simba imekubali yaishe kwa straika Laudit Mavugo kwamba haitampata tena, lakini imeweka mkakati wa kuhakikisha inamfuata Ufaransa ili arudishe fedha zao Sh milioni 36. Mwaka jana, Simba ilimpa Mavugo kiasi hicho cha fedha lakini kumbe ilikuwa sawa na bure kwani alikuwa na mkataba na Vital’O ambayo ilidai fedha ndefu ili imwachie straika huyo. Simba haikuwa na fedha hiyo ikaamua kutulia ikiamini straika huyo atajiunga nao pindi akimaliza mkataba na Vital’O, ajabu Mavugo alipomaliza mkataba akauchuna.

Kuona hivyo Simba ikamtuma kiongozi wake mmoja kumfuata Mavugo nchini Burundi, lakini bosi huyo akaishia kuonana na katibu wa Vital’O bila kumuona rais wa timu hiyo, Bikolimana Benjamini anayesimamia haki za straika huyo. Bosi huyo wa Simba akaamua kugeuza zake na kurudi Dar es Salaam huku nyuma Mavugo akipelekwa Ufaransa.

 

Habari kutoka Simba zinasema, klabu hiyo sasa imetegeshea Mavugo akisajiliwa tu Ufaransa watamfuatilia na kudai fedha yao Sh milioni 36 walizompa. “Mavugo hawezi kuja tena, kiongozi wetu mmoja aliyetumwa Burundi ameshindwa kuzungumza na rais wa Vital’O ambaye ndiye aliyegomea Mavugo kuja Simba. Kutokana na hali hiyo sasa tunasubiri fedha yetu. “Mavugo akipata timu Ufaransa tutamfuata na kudai fedha yetu, wala hatugombani naye,” alisema bosi huyo wa Simba.

Leave A Reply