The House of Favourite Newspapers

Simba, Yanga Kuanzia Dar

YANGA na Simba zitaanzia nyumbani kwenye mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Wanawake utakaoanza Machi 9.

Simba wataikaribisha Tanzanite kutoka Arusha huku Yanga wakianza na Alliance Girls kutoka Mwanza.

Kwa upande wa Yanga wao wamefanya usajili wa wachezaji tisa katika dirisha la usajili lililofungwa Februari 25, tofauti na Simba ambao wameongeza mchezaji mmoja tu, Everyine Oppa ambaye anacheza katika nafasi ya ushambuliaji. Katika msimamo wa michuano hiyo Simba Queens inashika nafasi ya tano ikiwa na pointi 22,Yanga wao ni wa saba wakiwa na pointi 13.

Comments are closed.