SPOTI XTRA LAZIDI KUJIPANUA KWA WASOMAJI
KIKOSI kazi cha kampuni ya magazeti ya Global Publishers Ltd, leo kiliingia tena mitaani kulinadi gazeti la Spoti Xtra ambalo limeanza kutoka kila Alhamisi kuanzia wiki iliyopita. Kikosi kazi hicho kiligawanyika sehemu mbalimbali za Jiji la Dar yakiwemo maeneo ya Makumbusho, Ubungo, Buguruni, Karume, Keko Tandika, Temeke na sehemu nyingine ambapo waliwauzia wasomaji gazeti hilo na kukusanya maoni yao.
Matukio katika Picha:
Msanifu kurasa wa Magazeti ya Global Publishers, Charles Mgela, akimuonesha gazeti mpita njia eneo la Keko-Veta jijini Dar.
PICHA: RICHARD BUKOS / GPL
Comments are closed.