The House of Favourite Newspapers

Suge Knight Akataliwa Kwenda Kwenye Maziko ya Mamake

UWEZEKANO wa prodyuza na mfanyabiashara wa masuala ya muziki wa Marekani, Suge Knight, kwenda kwenye maziko ya mama yake ambaye amefariki juzi (Jumapili) hospitalini, unazidi kuwa finyu kwa vile mamlaka ya magereza imesema haiwezi kumruhusu prodyuza huyo kwenda nje kwa vile anakabiliwa na kesi ya mauaji.

Mama yake Suge aliyekuwa anaitwa Maxine Chatman, alifariki kutokana na matatizo ya kiharusi.

Pamoja na habari kwamba huenda mtuhumiwa huyo akakata rufaa dhidi ya uamuzi wowote wa kumgomea asiende kwenye maziko hayo, bado inaaminika kwamba mahakama haitabadili uamuzi huo.

Comments are closed.