Taswira za sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar
Baadhi ya Maafisa mbali mbali wa Vikosi vya Ulinzi na Taasisi za Serikali wakiwa katika sherehe za kilele cha Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kutimia miaka 52 zilizofanyika katika uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja.
Vijana wa Chama cha Mapinduzi wakibeba Picha la Marehemu Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Karume wakati wa Maandamano ya kusherehehekea Kilele cha Mapinduzi Kutimia miaka 52.
Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mjini wakibeba mabango yenye ujumbe tofauti kama yanavyoonekana wakati wa Maandamano ya kusherehehekea Kilele cha Mapinduzi.