TECNO WAZINDUA TECNO Spark 4
KAMPUNI ya simu ya TECNO kwa kushirikiana na kampuni ya simu ya Tigo jana wamezindua simu mpya aina ya TECNO Spark 4 yenye sifa inayouzwa kwa bei nafuu sana.
Akizungumza na wanahabari kwenye uzinduzi wa simu hiyo uliofanyika katika duka la TECNO Spark Hub lililopo Kariakoo, Dar es Salaam, Meneja Masoko wa kampuni hiyo, William Motta, alisema teknolojia iliyopo kwenye simu hiyo inazipa uwezo kamera za nyuma GB 32 za memory na kioo cha nchi 6 full –view. Pia simu hizo betri zake zinadumu na chaji kwa muda mrefu.
Wakati huohuo Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo, Mkumbo Mnyonga, alisema wateja watakaponunua simu hiyo watazawadiwa ofa ya GB 18.
Matukio katika Picha:
HABARI/PICHA: NEEMA ADRIAN / GPL
Comments are closed.