Muimbaji mkongwe wa bendi hiyo, Luiza Nyoni (kushoto) na Kalala Juniour wakiwajibika kwa staili ya wapendanao.Kikosi cha Twanga kikiwajibika jukwaani.Mkali wa muziki wa mchiriku almaarufu kama Msagasumu naye alipewa nafasi ya kusindikiza onesho hilo.Mashabiki wakimtunza Msagasumu baada ya kuwakosha. Wapendanao hawa nao walinaswa wakijimwaya kwa raha zao.Wadau wa Twanga wakiwa kwenye picha ya pamoja na mtangazaji wa muziki wa dansi, Abdallah Zomboko mwenye maiki.Mkurugenzi wa Twanga, Asha Baraka akiwa na wanenguaji wake.
Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ usiku wa kuamkia jana, Jumapili ilifanya onesho la wadau wa bendi hiyo lililoitwa Jukwaa la Twanga ambalo lilifanyika Ukumbi wa Mango Garden jijini Dar.
Katika onesho hilo umati wa wadau hao ulipata burudani hiyo kuanzia nyimbo za albamu ya kwanza mpaka zinazotamba hivi sasa.
PICHA: RICHARD BUKOS / GPL
Comments are closed.