The House of Favourite Newspapers

UCHEBE: OLE WAKE NIMKUTE MTU NA SHILOLE

CHIMBA mkwara! Mume wa mwanamuziki wa miondoko ya mduara Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, Ashrafu Uchebe ametangaza vita kwa mwanaume yeyote ambaye atamkuta na mkewe kimapenzi kwani yuko tayari kwenda jela endapo atamkuta mkewe na mwanaume mwingine au kumfumania.

 

Akizungumza na Over Ze Weekend, Uchebe alisema kuwa anajua anapata tabu gani kuhakikisha anailinda ndoa yake hivyo ataumia sana atakapomkuta mwanaume mwingine anamrubuni mkewe na anaweza kufanya kitu ambacho hakikutarajiwa na watu wengi.

 

“Mimi nampenda sana mke wangu najua wazi ni kiasi gani naumia kuilinda ndoa yangu isiingiliwe na kidudu mtu ila watu hawezi kuelewa hata kidogo hivyo kama nitamkuta mwanaume yeyote au nikimfumania mke wangu huyo mwanaume ama zake ama zangu,” alisema Uchebe.

IMELDA MTEMA

Comments are closed.