Akizungumza nje ya ukumbi wa bunge mjini dodoma mara baada ya kutoka nje, Mbunge wa Vunjo na Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James Mbatia, amesema hawajatoka wala kulikimbia bunge, na kwamba wapo bungeni na wanaendelea kufanya kazi za bunge.
“Hatujakimbia bungeni, tunashiriki kwenye kamati, hatujasusia bunge, tumechukizwa, tunahasira na vitendo vya kibabe, vya kionevo vinavyofanywa na kiti.” Alisema Mbatia
jamani hakuna sheria ya hao wabunge?huu mchezo wa kutokatoka bungeni kwa nini wasiwatoe moja kwa moja wapo wwngi wanaohitaji kutumikia wannchi sio wai wanaopanga visa kl leo tumewachoka