The House of Favourite Newspapers

Uni-industries Tanzania Ltd Inawakaribisha kwenye Uzinduzi wa Duka Lao

David Laizer, Afisa Masoko wa Uni-industries Tanzania Ltd

Uni-industries Tanzania Limited ni kampuni kutoka Afrika Kusini ambayo wanafanya biashara ya bidhaa za ndani kama vile Majiko, Vifaa kwa ajili ya Supermarket, mashine za bakery pamoja na Mashine za Kufulia (Laundry Equipnment) pamoja na bidhaa za mahotelini.

Tarehe 6 na 7 mwezi August, 2018 watakuwa na ufunguzi rasmi wa Ofisi zao na  uzinduzi rasmi wa bidhaa zao kwa hapa Tanzania. Uzinduzi huo utafanyika katika Ofisi zao (Showroom) iliyopo barabara ya Haile Selasie, Mkabala na Marrybrown, Masaki Dar es Salaam.

Afisa Masoko wa Uni-industries Tanzania Ltd, Glory Loishie

Maafisa Masoko wa kampuni ya Uni-industries, Glory Loishie na David Laizer wametembelea studio za +255 Global Radio na kuelezea ubora wa bidhaa za kampuni ya Uni-industries. Wameeleza kuwa bidhaa zote zinazozalishwa na kampuni yao, zina ubora wa hali ya juu ambao unaendana na thamani ya pesa yako.

Katika uzinduzi huo, kutakuwa na maonyesho ya jinsi bidhaa zao zinavyofanya kazi, kama vile uokaji wa mikate na matumzi mengine kama utengenezaji wa juice, Jinsi ya kutumia Mashine za kufulia na nyingine nyingi. Katika siku hiyo ya uzinduzi, vyakula na vinywaji vyote vitatolewa bure. 

Watu binafsi na makampuni mbalimbali Wanakaribishwa sana siku hiyo ya uzinduzi, na Maonesho hayo yataanza saa tatu Asubuhi mpaka saa 11 Jioni, kwa siku mbili mfululizo Tarehe 6 na 7 Mwezi August, 2019 

Wasiliana Nao kwa Njia Zifuatazo

Simu : +255 766 075 031

E-mail : [email protected]

Website : www.uni-eastafrica.com

Comments are closed.