The House of Favourite Newspapers

Uwoya Atoa Sharti Kutazama ilamu zake

0
Irene Uwoya

STAA wa filamu Bongo, Irene Uwoya ametoa sharti kwa mashabiki wake kwamba kila wanapokuwa wanataka kutazama filamu zake hasa zile za mapenzi ni vema wakawa na rimoti karibu maana huwa anakuwa ‘deep’ katika kutekeleza ‘script’ inavyotaka, hivyo ni bora kuwa na rimoti kama kutakuwa na watoto
pembeni au watu wanaoheshimiana.

 

Akichonga na Staa Mix, Uwoya alisema kuwa, amekuwa akijituma ipasavyo katika screen za mapenzi kwa sababu ni miongoni mwa scene anazopenda kucheza kwenye filamu, kwa hiyo rimoti ni muhimu kwa watazamaji.

 

“Katika sanaa nasimamia mwongozo wa script, inapojitokeza suala la scene za mapenzi huwa nakamua vibaya sana, baadhi ya watu wanakwazika kwa namna ninavyocheza, lakini ushauri kwa wale wazazi ambao ni mashabiki wangu ni vema kila wanapotazama filamu zangu wawe karibu na rimoti ili kuondoa sehemu ambazo zinawakera,” alisema Uwoya.

Spoti Hausi: Said Maulid ‘SMG’ Ampa Mchongo Lwandamina

Leave A Reply