Vodacom Yasogeza Huduma kwa Wakazi wa Masaki Jijini Dar Es Salaam
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo (wa pili kulia) akikata utepe kuzindua duka jipya la kisasa la Vodacom lililopo mtaa wa Haile Selassie Masaki leo. Wengine ni Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Stella Msofe (wa pili kushoto), Mkuu wa Mauzo wa Vodacom kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Brigita Stephen na Msimamizi wa duka, Emmanuel Makaki. Uzinduzi wa duka hilo, utasogeza karibu huduma za kampuni hiyo kwa wateja wake.
Keki nayo ilikatwa katika kusherehekea uzinduzi huo.