The House of Favourite Newspapers

Wadau Mbalimbali Wakutanishwa Na Puma Energy kwenye Iftar

0
Mkurugenzi Mkuu wa Puma Energy Tanzania Fatma Abdallah akisalimiana na wageni waalikwa wakati wa hafla ya Iftar iliyofanyikaa jijini Dar es Salaam.

Dar es Salaam, 28 Machi 2024: KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika Iftar iliyoandaliwa na Kampuni hiyo huku ikitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania kuendelea kuwaunga mkono sambamba na kuhimiza kudumisha amani.

Hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Kampuni hiyo ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake Fatma Abdallah imefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa wadau mbalimbali wakiwemo wakuu wa taasisi za umma na binafsi pamoja na wateja wa kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania Dk . Selemani Majige akisalimiana na Mkurugenzi wa UDA-RT Waziri Kindamba pamoja na wageni wengine waalikwa waliohudhuria futari iliyoandaliwa na Kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.

Mgeni rasmi katika Iftar hiyo alikuwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Walid aliyewakilishwa na Sheikh wa Wilaya ya Temeke .

Akizungumza wakati wa Iftar hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni hiyo Dk Selemani Majige ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa ni vema kila Mtanzania kwa nafasi yake kuendelea kuliombea Taifa sambamba na kumuunga mkono Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.

“Tunafahamu kwa sasa tunaendelea na Mfungo wa Ramadhan pamoja na Kwaresima hivyo wakati tukiendelea na Mfungo ni vema tukaliombea Taifa letu lakini wakati huo huo kudumisha Umoja,amani na mshikamano,”amesema Dk Majige.

Amesisitiza kuendelea kudumisha amani katika nchini Kunafanya uchumi Wetu kuendelea kuimarika na biashara zetu ziendelee vizuri.”Kulinda amani ni jambo kubwa kwani kama hakuna amani basi hata biashara haziwezi kufanyika vizuri.

“Hivyo kupitia mwezi mtukufu wa Ramadhan ni vema kuendelea kumuomba Mungu na kuendelea kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ili aendelee kutuongoza na kudumisha amani katika taifa letu.”

Pia amewaomba Watanzania kuendelea kutumia mafuta ya Puma Energy Tanzania pamoja na bidhaa zake zote huku akifafanua mafuta ya Kampuni hiyo yana ubora na viwango vya hali ya juu.

“Tunawaomba muendelee kutumia mafuta ya Puma ili tuongeze faida na tukiongeza faida Serikali inapata gawio na inapotoa gawio zinapatikana fedha ambazo zinakwenda kuhudumia jamii katika maeneo mbalimbali,”

Kwa upande wake Sheikh wa Wilaya ya Temeke Sheikh Zailai Hassan Mkoyogole aliyemwakilishwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Omar aliyekuwa mgeni rasmi, amesema kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan jambo kubwa ni kuzidisha wema kwa maana wanadamu ni wakosaji mbele za Mwenyezi Mungu.

“Binadamu anamkosea Mwenyezi Mungu kwa vitu vingi hivyo sasa ameleta Mwezi mtukufu wa Ramadhan ili kutubu kwa yale yote ambayo ameyafanya.Hivyo kinachotakiwa katika mwezi huu ni kufanya yale yaliyomema na kurejea kwake,”

Pia amesema Mwenye Mungu anapenda kuombwa ,hivyo ametoa mwito kwa watu wote kurejea kwa Muumba kuomba msamaha.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa Puma Energy Tanzania Fatma Abdallah amewashukuru wadau waliojitokeza katika futari hiyo huku akitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania kuwaunga mkono kwa kununua bidhaa za mafuta ya Kampuni hiyo.

Aidha amesema wao kama Puma Energy Tanzania wataendelea kuunga mkono juhudi za Serikali hasa katika kutekeleza matumizi ya nishati safi ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa lengo la kuendelea kutunza mazingira .

“Puma Energy Tanzania tunatambua mwelekeo wa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na hasa kwenye suala la nishati safi hivyo tutaendelea kuaidia kwa lengo la kuhakikisha mazingira yanalindwa na matumizi ya nishati safi kwa watanzania yanakuwa kipaumbele.”

Wakati huo huo Mkurugenzi Mkuu UDA- RT Waziri Kindamba aliyeshiriki futari hiyo amewapongeza kwa kuandaa futari hiyo ni kuwaalika wateja wao ambao wanatumia vilainishi na mafuta.

Leave A Reply