Waimbaji wa Injili wamfuta machozi Cassian!
MSANII wa nyimbo za Injili nchini ambaye pia ni mlezi wa waimbaji wa injili Tanzania, Emmanuel Mbasha ameeleza jinsi yeye na waimbaji wenzake walivyomfuta machozi msanii mwenzao Pascal Cassian ambaye alipata ajali ya gari siku za hivi karibuni.
MSHINDI BSS ALIA! “Niokoeni jamani, yaliyonikuta sitasahau”
Akizungumza na Ijumaa Wikienda Mbasha alisema kuwa, walichokifanya ni kuchangishana pesa na kumnunulia msanii huyo mahitaji mbalimbali lakini kubwa ni kumpatia Bima ya Afya ili aweze kutibiwa kwa urahisi tatizo lake la kibofu cha mkojo alilonalo.
“Tuliguswa na hali yake ya kiafya tukaona tufanye kile kilicho ndani ya uwezo wetu, tumempatia bima ya afya lakini pia tumempa vitu mbalimbali ambavyo vitamsaidia katika kipindi hiki kigumu anachopitia,” alisema Mbasha.
STORI: Memorise Richard, Ijumaa Wikienda.
Comments are closed.