The House of Favourite Newspapers

WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WAWAZAWADIA WAFANYAKAZI WA GLOBAL GROUP

Glory akisalimiana na Mhariri Mtendaji wa Global Group, Saleh Ally.

Katika kusherehekea Sikukuu ya Wapendanao, maafisa kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania jana walitoa zawadi kwa wafanyakazi wa Kampuni ya Global Group inayozalisha Magazeti ya Uwazi, Ijumaa, Amani, Risasi, Ijumaa Wikienda, Championi, Spoti Xtra pamoja na kumiliki Global TV Online.

 

Maafisa hao wakikabidhi zawadi ya dumu la asali kwa meneja wa Global, Abdallah Mrisho.

Zawadi hiyo ambayo ni dumu la lita tano la asali halisi ilikabidhiwa na Meneja Mawasiliano wa taasisi hiyo, Glory Mziray na afisa habari wake, Tulizo Kilaga kwa Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Abdallah Mrisho.

Maafisa hao wakiteta na Mhariri wa Gazeti la Championi, Elius Kambili.

 

Akizungumzia zawadi hiyo, Glory alisema kuwa, wameamua kuitoa ikiwa ni kuonesha upendo wao kwa wafanyakazi wa Global na kuimarisha ushirikiano mwema na vyombo mbalimbali vya habari nchini.

 

Maafisa hao wakizungumza na Abdallah Mrisho ofisini kwake.

“Tumefanya hivi kwa vyombo mbalimbali vya habari ikiwa ni katika jitihada zetu za kujenga ushirikiano mwema, tunajua umuhimu wenu katika sekta ya misitu hivyo tunaamini tutazidi kushirikiana katika mambo mbalimbali.

Mhariri Kiongozi wa Magazeti Pendwa, Amran Kaima (Mwenye tisheti ya njano) akiwatambulisha maafisa hao kwa baadhi ya wafanyakazi wa Global.

 

“Lakini pia tupo kwenye msimu wa wapendanao, tunawapenda na ndiyo maana tumeamua kuwaletea zawadi hii,” alisema Glory.

Mhariri Mtendaji wa Global Group, Saleh Ally akizungumza na maafisa hao ofisini kwake

 

PICHA NA MUSA MATEJA | GLOBAL PUBLISHERS

Comments are closed.