The House of Favourite Newspapers

VILANISHI VYA MAGARI, NDEGE VYAINGIA NCHINI

Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Faraja Mkinga, akionyesha bidhaa zao baada ya kuzizindua.
Ofisa Masoko wa Liqui  Moly, Angelina Ndege,  akionyesha bidhaa hiyo.
Ofisa Masoka na Mauzo wa kampuni hiyo, Clara Mkwama,  akionyesha bidhaa za kampuni yake.
Warembo wakishikilia chupa cha vilainishi hivyo wakati wa uzinduzi wa oili hiyo.
Baadhi ya wageni waalikwa katika hafla hiyo wakifuatilia kilichokuwa kikiendelea.

 

KAMPUNI ya Liqui Moly imeingiza bidhaa mpya za  oili  na vilainishi vya magari na mitambo kutoka nchini Ujerumani.

 

Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa Kampuni ya Liqui Moly, Faraja Mkinga, alisema kampuni yake ina fahari kubwa kuwapatia Watanzania bidhaa zenye ubora  wakati taifa likijipanga kuelekea katika uchumi wa kati.

 

“Bidhaa zetu ni za  ubora wa hali ya juu, zinapatikana katika bei inayoendana na hali ya uchumi.  Zipo za aina tofauti kama vilainishi vya magari madogo, magari ya usafirishaji, meli, majenereta, pikipiki na hata ndege.

 

Ameongeza kuwa kwa sasa bidhaa hizo zinapatikana jijini Dar es Salaam kwenye ofisi zilizopo Mikocheni B  na mawakala mbalimbali na kwamba humsaidia mteja  kupunguza gharama za uendeshaji wa magari na mitambo.

 

“Kampuni imeingiza oili itakayomwezesha mdau kutumia chombo chake hadi kilomita 15,000 tofauti na oili nyingine hapa nchini zinazoenda kilomita 3,000 mpaka 9,000 tu.

 

 

Comments are closed.