The House of Favourite Newspapers

WAKAZI KIGAMBONI WAMWANGUKIA RAIS MAGUFULI

Sehemu ya wananchi wakiwasikiliza viongozi wao.
Wananchi wakiwa eneo la shamba linalodaiwa kumilikiwa na mkurugenzi huyo.
Diwani wa Kata ya Somangila, Chichi Masanja (aliyesimama kulia) akizungumza na wananchi wake.
Viongozi wakiwasikiliza kwa makini wananchi.
Eneo la daraja linalodaiwa kujengwa na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini  (TARURA) kwa ajili ya kupitisha barabara hiyo.

 

 

WAKAZI wa  Kata ya Somangila  wilayani Kigamboni mkoani Dar es Salaam  wamemuomba  Rais  John Magufuli  na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda,  kuingilia kati suala la mgogoro uliopo kwenye kata hiyo uliokwamisha miundombinu ya barabara.

 

Hayo yamebainishwa na wakazi wa eneo hilo wakati wakizungumza na waandishi wa habari walipokuwa wamekutana na  Diwani wa Kata hiyo, Chichi Masanja na Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo, Sadick Mohamed, ambapo wameelezea kuhusu kero yao ya miundombinu ya barabara ambayo imekwamishwa na mmoja wa wakurugenzi wa halmashauri za mkoa mmoja hapa nchini.

 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi hao wameelezea kwamba mkurugenzi huyo (wakamtaja )  amezungushia uzio kwenye eneo la barabara, hivyo kusababisha usumbufu hasa kwa akina mama wajawazito wanapohitaji kwenda kujifungua.

 

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo kijiji cha Dege Kata ya Somangila, Sadick Mohamed, amesema kuwa mkurugenzi huyo amejimilikisha zaidi ya ekari 100 ambazo haziendelezwi na hivyo zimesababisha kuwepo kwa wahalifu wanaojificha kwenye vichaka vilivyopo kwenye mashamba hayo.

 

Amesema kuwa mbali  na wahalifu pia amekwamisha miradi ya maendeleo kama vile ujenzi wa barabara unaosimamiwa na TARURA ambayo tayari fedha zake zilikwishatengwa katika bajeti ya 2017/18 hivyo ujenzi huo ukiendelea kusimama fedha hizo zinaweza kurudi serikali kuu.

 

Wakati huohuo, Masanja amesema ni vyema Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda aingilie kati suala hilo kwani linakwamisha maendeleo katika wilaya hiyo.

 

Comments are closed.