The House of Favourite Newspapers

WAKAZI WA SALANGA WALALAMIKIA UBOVU WA BARABARA YA KING’ONGO-KIMARA

Bajaj ikipita kwa tabu katika miundombinu hiyo.
Wananchi wa  Kimara Matosa wanaopita katika barabara ya King’ongo kuelekea maeneo ya Goba jijini Dar es Salaam wakisambaza kifusi.
Daladala ya Kimara-Matosa ikipita kwa tabu katika miundombinu hiyo.
Diwani wa kata ya  Saranga, Haruna Yusuf  Mdoe (katikati) akiwa ameungana na wananchi kusambaza kifusi.
Diwani wa kata ya  Saranga, Haruna Yusuf Mdoe (katikati mwenye sululu) akisambaza kifusi katika barabara hiyo.
Wakazi wa King’ongo kuelekea maeneo ya Goba jijini Dar es Salaam wakisambaza kifusi katika miundombinu hiyo ya barabara.
Taswira ya miundombini hiyo barabara ya King’ongo kuelekea maeneo ya Goba jijini Dar es Salaam.

 

 

WAKAZI wa Kimara Matosa wanaopita katika barabara ya King’ongo kuelekea maeneo ya Goba jijini Dar es Salaam, wamelalamikia kero ya ubovu uliokithiri wa barabara hiyo, inayowasababishia adha kubwa, hasa kipindi cha mvua.

 

Wakizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi la kujaza kifusi kwenye maeneo korofi kwa kushirikiana na diwani wa Kata ya Saranga, Haruna Yusuf wananchi wa eneo hilo, wamesema barabara hiyo imekuwa kero kubwa kwao kutokana na kuwa na mashimo makubwa, hali inayosababisha watumie muda mrefu kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

 

Naye diwani wa kata hiyo, Haruna Yusuf Mdoe aliyekuwa akishirikianana wananchi wake kumwaga kifusi kwenye maeneo yenye mashimo makubwa, amewaomba wadau mbalimbali kusaidia kurekebisha barabara hiyo ili kutatua kero hiyo inayowatesa wananchi wake.

 

NA DENIS MTIMA/GPL

Comments are closed.