WALIOKATAA FEDHA ZA UWOYA GLOBAL WAPEWA KITITA
UONGOZI wa Global Publishers umewapongeza kwa kuwapa kitita cha fedha wanahabari wake, Imelda Mtema na Hillary Daudi, kwa kuonesha weledi wa kutogombea fedha wakati mwigizaji wa Bongo Movies, Irene Uwoya alipowamwagia fedha waandishi wa habari waliojitokeza katika Ukumbi wa Hyatt Kilimanjaro jijini Dar, hivi karibuni kwenye mkutano ulioitishwa na wasanii wa tasnia ya filamu nchini.
Tukio hilo la Uwoya lilielezwa kuwa la kidhalilishaji kwa waandishi ambao walipigana vikumbo kugombea fedha za msanii huyo.
Comments are closed.