The House of Favourite Newspapers

Wamiliki wa Magari Kenya Waingia Tanzania Kununua Mafuta ya Bei Rahisi

0

Maelfu ya wamiliki wa magari pamoja na waendesha boda boda katika mji wa mpakani wa Namanga wanaendelea kuingia nchini Tanzania ili kununua mafuta ya bei rahisi kulingana na gazeti la Nation.

Tarehe Mosi mwezi julai shirika la kudhibiti bei ya mafuta nchini Kenya EPRA liliongeza bei ya mafuta kwa mujibu wa sheria ya fedha ya 2023, ambayo iliongeza VAT kutoka asilimia 8 hadi kumi na sita

Mjini Nairobi na kaunti ya Kajiado lita moja ya petroli inauzwa kwa shilingi 195.5 za Kenya huku nchini Tanzania ikiuzwa kwa shilingi 2,781 za Tanzania ambazo ni shilingi 160 za Kenya.

Hii ina maana kwamba lita moja ya mafuta ya petroli iko chini kwa shilingi 35 za Kenya nchini Tanzania.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti la Nation Media, umebaini kwamba wengi waliokuwa wakinunua mafuta katika kituo cha mafuta cha Admire Filling Station kilichopo kilomita moja kutoka mpakani ni raia wa Kenya.

Kulingana na gazeti hilo, bei ya mafuta imekuwa ikishuka nchini Tanzania katika kipindi cha miezi miwili iliopita huku ikipanda nchini Kenya.

#EXCLUSIVE: MSANII ANAYEDAI KUIBIWA WIMBO na ANJELLA AIBUA MAZITO, ALIVYOFOKEWA, AELEZA KWA UCHUNGU

Leave A Reply