Wanandoa Washangaza Kwa Kukataa Kupata Watoto Kwenye Ndoa Yao…
WANANDOA wawili kutoka huko Orange County California Marekani Taylor Vasu (28) na mume wake Justin (27) wamejikuta waki-trend maeneo mbalimbali nchini humo baada ya kujitokeza hadharani na kudai kuwa hawataki wala hawatarajii kuja kuwa na watoto kwenye ndoa yao, licha ya kudumu kwenye ndoa miaka 6 mpaka sasa hivi.
Taylor na Justin wanadai kwamba kitendo cha kupata watoto kitawafanya wawe ni watu wenye huzuni muda wote, kitu ambacho hawataki kiwatokee kwenye maisha yao yote.
“Tunaona maisha ya watu wenye watoto yalivyo, ni huzuni tu muda wote hatutaki maisha hayo”- alisema Taylor (Mke) kwenye mazungumzo na Daily Mail.