WASTARA HALI TETE TENA !
LICHA ya Februari, mwaka huu kupatiwa matibabu nchini India, bado hali ya staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma ni tete kwani yu hoi kitandani akisumbuliwa na kichwa pamoja na mgongo.
Akizungumza na Za Motomoto News, Wastara alisema yupo kwenye mateso makubwa ya maumivu ya kichwa na mgongo na tarehe ya kurudi hospitali nchini India imeshafika lakini ameshindwa kwenda kutokana na kukosa fedha za matibabu.
“Dawa nimemaliza na muda wa kurudi hospitali umefika lakini sina fedha mpaka sasa, nimefuatilia fedha za kazi niliyofanya na Wahindi walionisainisha mkataba wa kuwa balozi wa simu zao lakini mpaka leo hawajanilipa chochote na wametoroka, nimechanganyikiwa tu hapa, namuomba Waziri Harrison Mwakyembe (Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo) anisaidie ili nipate haki yangu niweze kwenda kutibiwa,” alisema Wastara.
Comments are closed.