The House of Favourite Newspapers

Waziri Mkuu akabidhi kombe  timu ya Mpira wa Kikapu ya  NMB

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya soka ya Bunge, Cosato Chumi baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa 5-3 dhidi ya timu ya NMB katika Bonanza la Benki ya NMB na Wabunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.
…Majaliwa akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya Mpira wa Kikapu ya Benki ya NMB, Danford Kisinda baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa vikapu 54-52 dhidi ya timu ya mpira wa Kikapu ya Bunge. 
Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Tulia Akson mwenye Miwani Nyeusi mbele na Mkurugenzi wa Benki ya NMB pamoja na timu ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wakifurahia ushindi wa timu za bunge kwenye Bonanza la michezo la NMB na Bunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.
Mkurugenzi wa Benki ya NMB akishangilia ushindi wa Mpira wa Kikapu baada ya kuwashinda timu ya Bunge kwa Vikapu 54 kwa 52 kwenye Bonanza la michezo la NMB na Bunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.

 

 

 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesifu juhudi za Benki ya NMB kwenye kuunganisha jamii kupitia huduma bora za kibenki, matukio ya michezo na hata misaada mbalimbali nia ikiwa kuona jamii ya kitanzania inashiriki kikamilifu kwenye ujenzi wa Taifa.

 

Alitoa kauli hiyo juzi jijini Dodoma kwenye Bonanza la michezo lililowashirikisha wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wafanyakazi wa Benki ya NMB.

 

Akizungumzia kuhusu utendaji wa benki ya NMB, amesema imekuwa ikishirikiana na Serikali kuwaelimisha wakulima umuhimu wa kufungua akaunti na kujiwekea akiba.

 

“Benki ya NMB ni benki pekee iliyomudu kufungua matawi hadi maeneo ya vijijini, hivyo kurahisishha upatikanaji wa huduma kwa watumishi na wananchi waishio maeneo hayo.”

Amesema ni muhimu kwa watumishi kushiriki katika michezo mbalimbali kwa kuwa inaimarisha afya pamoja na kudumisha mshikamano.

Michezo iliyochezwa katika bonanza hilo ni mpira wa miguu ambapo timu ya Bunge ilishinda baada ya kuifunga timu ya benki ya NMB magoli matano kwa matatu.

Kwa upande wa mchezo wa mpira wa pete timu ya Bunge iliibuka na ushindi baada ya kuifunga timu ya NMB magoli 25 kwa 18, huku katika mchezo wa mpira wa kikapu timu ya NMB ilishinda baada ya kuifunga Bunge vikapu 54 kwa 52.

Katika mchezo wa kuvuta kamba timu ya Wabunge Wanawake na Wanaume waliibuka na ushindi baada ya kuzishinda timu za NMB.

Comments are closed.