WEMA APOKELEWA KWA SHANGWE NA WAHARIRI GLOBAL (PICHA + VIDEO)
MWIGIZAJI maarufu wa Bongo Movie, Wema Sepetu, leo Ijumaa, Julai 26, 2019, amepokelewa kwa shangwe na wahariri wa Global Publishers, wachapishaji wa Magazeti ya Ijumaa Wikienda, Uwazi, Risasi, Amani, Ijumaa, Championi na Spoti Xtra, Sinza-Mori jijini Dar es Salaam alipokuja kutambulisha ujio wake mpya wa ‘Wema Empire’ ambao utahusika na uandaaji wa filamu nchini.
Mrembo huyo amesema Julai 27, 2019, itakuwa siku atakayofanya usaili (audition) wa kusaka vipaji vya waigizaji utakaofanyika katika Viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam ambao wakakaofaulu, utawawezesha kupata fursa ya kushiriki kwenye tamthilia mbalimbali ambazo zitaandaliwa chini ya himaya yake.
Usaili huo utakaofanyika saa 4 asubuhi hadi saa 10 jioni utahusu wanaume wenye kuanzia miaka 26 hadi 35, wanawake miaka 22-30, kinababa miaka 45-60 na kinamama miaka 45-60.
Comments are closed.