The House of Favourite Newspapers

WEMA: MAPOVU YAMEWATOKA KAMA YOTE

Wema Isaac Sepetu

STAA wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu amewafungukia watu ambao wanamsema maneno ya kashfa kufuatia kumuanika mumewe mtarajiwa, Patrick Christopher ‘PCK’.

Wema aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, yeye ana uamuzi wake binafsi wa kufanya anachotaka kwenye maisha yake, lakini anashangaa watu wengine wanamuingilia mpaka kwenye maisha yake binafsi na kutokwa povu. “Yaani watu wametokwa na povu kama lote, kisa tu mimi kumuonesha mwanaume wangu, sasa hata wakiungana dunia nzima kunisema, kama nimeshampenda watanibadilisha vipi?” alihoji Wema.

Wiki iliyopita ulizuka mjadala mzito kwenye Mtandao wa Kijamii wa Instagram baada ya Wema kutupia picha ikimuonesha akiwa kitandani na mwanaume huyo na kuweka wazi kuwa ndiye mumewe mtarajiwa.

STORI: Imelda Mtema, DAR

Comments are closed.