The House of Favourite Newspapers

Wema: Nt’aachika Kwa Mengine Sio Mapishi

0


WEMA Sepetu amesema kuwa hana wasiwasi kwenye kumridhisha mwanaume atakayekuja kuwa mumewe katika kipengele cha mapishi, kwani yupo vizuri.

 

Akizungumza na Risasi Vibes, Wema ambaye amefanya makubwa kunako anga la Bongo Muvi, alisema kuwa kitu ambacho anajivunia kutoka kwa mama yake ni kwamba, alimfundisha jinsi ya kupika kila kitu kama mwanamke.

“Kwa kweli mimi najua wanaume wengi wanapenda sana msosi, sasa mimi hakuna msosi ambao unanishinda kupika au vitafunwa vyovyote, sasa mwanaume akinioa labda aniache kwa sababu nyingine tu na si kwamba mambo ya jikoni, niko vizuri,” alisema Wema.

Leave A Reply