The House of Favourite Newspapers

YALIYOJIRI MIAKA 20 YA TWANGA

Mkurugenzi wa Twanga Pepeta, Asha Baraka (kulia) na Katibu Mtendaji wa Basata, Godfrey Mungereza,  wakikata keki ya ya kuadhimisha miaka 20 tangu kuanzishwa kwa bendi hiyo.

USIKU wa kuamkia leo Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ imefanya tamasha la kutimiza miaka 20 tangu ianzishwe ambapo umati wa mashabiki na wadau wake walifurika kwenye Viwanja vya Life Club, Mwenge jijini Dar.

Katika tamasha hilo, bendi hiyo ilianza na kutumbuiza kwa nyimbo zake zilizoanza kutamba yangu enzi hizo na mpya. Sambamba na kutumbuiza,  ilitolewa historia ya bendi hiyo iliyopitia milima na mabonde mpaka kufikia ilipo sasa.

Matukio katika Picha:

Asha Baraka akimlisha Mungereza keki.

                     Hivi ndivyo wanamuziki wa bendi hiyo walivyoibukia jukwaani kininja.

Muimbaji wa Twanga, Chalz Baba,  akiwajibika.

Mama Mondi (mwanamuziki Diamond) na ‘Anko’ nao walikuwepo.

 Kalala Junior (kushoto) na Haji Ramadhani wakishtua ‘kijotijoti’.

Msafiri Diouf (kushoto) akiongoza mashambulizi.

                    Meneja wa Wasafi Classic Baby (WCB), Bab Tale (kulia) na wasanii wa filamu za Bongo, Steve Nyerere (katikati)  na JB wakiwaburudisha mashabiki kwa maneno ya ucheshi.

                     Wanenguaji wa Twanga wakiwa kazini.

Mwanamuziki mwenye miaka 20 kwenye bendi hiyo, Luiza Nyoni akiimba.

                       Mashabiki wakijimwaya.

PICHA: RICHARD BUKOS / GPL

Comments are closed.