The House of Favourite Newspapers

Yanga Hii Inahitaji Huruma Maalum, Vinginevyo Aibu

UNAWEZA kudhani kama ni mchezo wa kui­giza kuona klabu kubwa inaingia kwenye mapito magumu ya kiuchumi, Kiutawala na kiuchezaji na mara nyin­gi jambo hili linapotokea basi utaona taswira nzima ya uendeshaji wa kla­bu inayumba na kupoteza muelekeo.

 

Yanga na Simba ndizo klabu zi­nazotajwa kuwa kubwa hapa nch­ini lakini usifikiri kwamba ukubwa unaozungumzwa unalenga moja kwa moja kwenye maendeleo ya­nayotakiwa kuwepo kwenye klabu yenye hadhi ya ukubwa la hasha! hapa unatajwa ukubwa wa kuzaliwa.

 

Yanga imezaliwa au kuanzishwa mwaka 1935 na Simba ikaanzishwa mwaka mmoja baadae yaani mwa­ka 1936, hapa utakubaliana nami kwamba hizi ndizo klabu kongwe ku­liko zote zilizopo katika nchi yetu.

 

Klabu hizi kubwa zimekuwa na mfanano wa kiuendeshaji kwakuwa zote zinatumia mfumo wa wanach­ama katika maamuzi makubwa ya­nayohusu klabu,hivyo mara nyingi utaona jambo linapojitokeza Yanga linaweza kujitokeza pia upande wa Simba,na ndiyo sababu klabu hizi zimepachikwa jina la Kurwa na Doto.

 

Hebu sasa turudi kwenye lengo kuu la makala haya,klabu ya Yanga kwa sasa inaonekana kupoteza muelekeo kwa kiasi kikubwa hasa kutokana na kuka­biliwa na mvurugano wa kiuendeshaji unaosababishwa na makundi yaliyo­jitengeneza ndani ya klabu hiyo yenye wanachama na mashabiki wengi ku­liko klabu nyingine yeyote hapa nchini.

 

Kuwepo kwa makundi yanayohusi­sha wanachama pamoja na viongozi waliochaguliwa na kuteuliwa ni kas­umba iliyojengwa kwa miaka mingi kiasi cha kufanya klabu kushindwa ku­jipambanua kimataifa na badala yake huishia kutamba tu hapa nyumbani licha ya kuwa na wachezaji wa kigeni wanaowasajili kwa gharama ya kufuru.

 

Baada ya kuukosa ubingwa wa msimu uliomalizika ambao umechuku­liwa na majirani zao Simba,Yanga ilianza kubomoka taratibu kuanzia kwenye kamati ya usajili ambayo ilijisahau na kujiona kuwa yenyewe ndiyo yenye jukumu la mwisho ka­tika maamuzi, kana kwamba hawajui kuwa ipo kamati ya utendaji juu yao il­iyokabidhiwa majukumu ya uratibu na utekelezaji kwa matakwa ya kikatiba.

 

Kwa mujibu wa katiba ya Yanga, kamati ya usajili kazi yake kubwa ni kusikiliza na kupokea mapendekezo au maagizo ya benchi la ufundi kuhusu kuongeza au kuwaondoa wachezaji fu­lani kikosini na baada ya hapo Kamati inapeleka mapendekezo hayo kwenye kamati ya utendaji kwa utekelezaji.

 

Hivi karibuni Abbas Tarimba am­baye ni mwenyekiti wa zamani wa Yanga,alikabidhiwa uongozi wa kamati ya usajili kwa lengo la kuis­uka upya klabu hiyo iliyobomoka lakini cha kushangaza likaibuka kundi linalotajwa kukereketwa na maendeleo ya klabu likapinga ua­muzi huo naye kuamua kujiuzulu.

 

Uchunguzi makini wa makala haya umebaini kwamba kundi hilo lililo­changanyika na watu waliomo kwenye kamati hiyo hapo kabla limepinga uamuzi wa mkutano mkuu kuikabidhi kamati mikononi mwa Tarimba,kwa kile kinachotajwa kuwa huenda aka­ziba mirija waliyokuwa wakiitumia kupitishia 10% za usajili, kutokana na msimamo madhubuti alionao.

 

Kwa hali ilivyo sasa nadhani Yanga inahitaji ‘huruma maalum’ ili kuiokoa katika mapito magumu inayopitia wakati huu ambao inahitaji kufanya usajili wenye kiwango na siyo kusajili wachezaji magarasa walioshindwa kuwika kwenye klabu walizotoka.

 

Niwape ushauri wa bure nyie wanayanga,njia pekee ya kuirudi­sha klabu yenu kwenye mstari ni kuitisha mkutano mkuu wa dharura na kufanya maamuzi magumu ka­tika safu nzima ya uongozi kwa ku­waondoa wasiofaa na kuwabakiza wenye uchungu wa kweli wa mata­tizo wa klabu bila kumuonea mtu.

 

Na baada ya hapo hakikisheni kwa pamoja mnavunja makundi yaliyopo na kuwa pamoja, mkizun­gumza lugha moja na hatimaye kuilinda klabu isivamiwe tena na viongozi mizigo kwa kuwa tayari mtakuwa mmesha wabaini,kinyume na hapo mtapata tabu sana.

NA OMARY KATANGA | CHAMPIONI JUMAMOSI

Comments are closed.