The House of Favourite Newspapers

Yanga Princess wanarudi kivingine

KOCHA wa Yanga Princess, Mohamed Hussen amesema wanarudi na sura ya tofauti katika raundi hii ya lala salama ya ligi kuu ya Wanawake iliyoanza kutimua vumbi jana.

Yanga Princess, walianza ligi hiyo kwa kusuasua na kujikuta wakiambulia ushindi mara sita,
wakipigwa mara saba na kutoa sare moja, huku wakishika nafasi ya saba kabla yamchezo wa jana dhidi ya Alliance.

 

Hussen aliliambia Spoti Xtra kuwa; “Unajua tulikuwa wageni kwenye ligi, hali ambayo ilikuwa inatupa changamoto sana, ila kwa sasa tumeimarika na nina imani tutanya vizuri katika hatua hizi za mwisho.”

SERENGETI BOYS Kufungwa ( 3 – 0), Wadau wa SOKA Wanasemaje?

Comments are closed.