The House of Favourite Newspapers

YANGA YAMNASA MBADALA WA DONALD NGOMA KUTOKA BENIN

Msham­buliaji wa timu ya Taifa ya Benin na Klabu ya Buffles du Borgou FC ya nchini huko, Marce­lin Degnon Koukpo.

 

YANGA ni kama imejibu mashambulizi baada ya juzi usiku kumshusha msham­buliaji wa timu ya Taifa ya Benin na Klabu ya Buffles du Borgou FC ya nchini huko, Marce­lin Degnon Koukpo na jana usiku alitarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili.

 

Vigogo wa Yanga wam­emshusha mchezaji huyo ambaye inadaiwa kwamba ndiye mbadala wa Amissi Tambwe ambaye inaoneka­na maji yamezidi unga na huenda wakaachana nae kama ilivyokuwa kwa Don­ald Ngoma aliyetua Azam kwa Hans van Der Pluijm.

 

Tambwe alikuwa akiwa­kosha Yanga kutokana na uwezo wake wa kutupia hata kwa vichwa ambavyo Mbenin huyo amewaambia viongozi kwamba hiyo ni kazi ndogo kwake kwani amekuwa akiifanya marany­ingi.

Marcelin alitua nchini juzi Alhamisi usiku akitokea kwao Benin kwa ajili ya kumalizana na Yanga akiwa kama mchezaji huru na kama mambo yamekwenda sawa jana huu utakuwa ndiyo usajili wa kwanza wa Kocha Mkongomani, Mwinyi Zahera.

Mbenin huyo mwenye mi­aka 23, tofauti na uwezo wa kupiga vichwa, pia viongozi wa Yanga wanadai wameam­biwa na kocha kwamba ana uwezo wa kupiga mashuti ya mita 20.

 

Yanga ambayo bado haijaimarika kiuchumi, inafanya maboresho katika safu ya ushambuliaji haswa kutokana na kuwepo kwa uwezekano wa Mzambia, Obrey Chirwa kuibukia Simba kuchukua nafasi ya Laudit Mavugo ambaye ameshaam­biwa kwamba hana chake.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo Championi Juma­mosi imezipata, mshambuliaji huyo hadi anatua nchini alikuwa tayari ameshamali­zana na vion­gozi wa Yanga na imebaki kutia dole gumba tu na kwenda Kenya ku­ungana na wenzake wa­naoshiriki michuano ya SportPesa inayoanza kesho.

 

“Hadi anakuja hapa nchini mshambuliaji huyo viongozi walikuwa wamemalizana kila kitu ikiwemo dau la usajili na muda wa mkataba am­bao yeye alifikia makubal­iano mazuri ya kusaini.

“Hivyo, mshambuliaji huyo anasaini mkataba leo usiku (jana) na kesho (leo) asubuhi anatarajiwa kupanda ndege kwenda Kenya kujiunga na wen­zake kwenye michuano ya SportPesa,” kilisema chanzo chetu.

 

Mwenyekiti wa Kamati Usajili wa Yanga, Hus­sein Nyika jana jioni hakupatikana kufafanua lakini Championi linajua kwamba mchezaji huyo ameletwa kwa ushiri­kiano na Kocha Mwinyi Kaheza.

Alhamisi iliyopita Nyika alisikika akisema wamepan­ga kufan­ya usajili mkubwa ambao utashangaza wengi na hawakurupuki kwenye mipango yao.

Comments are closed.