The House of Favourite Newspapers

Yusuf Manji Alikuwa Hafai, Ajabu Waliompinga Wameingia Mitini!

0
Aliyekuwa Mwenyekiti wa timu ya Yanga, Yusuf Manji.

INAWEZEKANA hii ikawa ni zaidi ya mara ya 50 au hata ikifika mara 100 kwangu nitaona sawa tu kama somo likiendelea ku­toeleweka kusema kuwa soka la sasa ni biashara, nitaen­delea kurudia tu kwa kuwa kuna watu wanalijua hilo lakini wanafanya makusudi kuzuia kwa faida zao binafsi.

 

Wakati Yusuf Manji al­ipokuwa akianza mchakato wa mabadiliko ya uendeshaji wa Klabu ya Yanga alikugusia pia juu ya umiliki wa klabu hiyo, kauli yake ilikuwa ni kama kisu kwa baadhi ya watu, wapo wa­liompinga kwa nguvu kubwa.

 

Mimi nilikuwa mmoja wa watu waliounga mkono ma­badiliko ndani ya Yanga na niliwahi kuandika hapa kuwa lolote ambalo litafanyika kipindi hicho hasa kama l i t a h u s i s h a m a b a d i l i k o ya kimfumo lazima liwe na kasoro, hivyo i t a t e g e m e a wahusika wa­tazitumia vipi hizo kasoro zao kufanya m a b o r e s h o ya kile wa­nachokitaka.

 

Yanga na Simba ni kla­bu kubwa na zenye nguvu kubwa ndani ya Tanzania, huwezi kuse­ma unabadili­sha mfumo wa uendeshaji kisha nda­ni ya muda mfupi kila kitu kinakaa sawa, hasa kwa kuwa kuna watu wanazitumia kuende­sha maisha yao ya kila siku.

 

Manji ni mfanyabiashara nilieleza hata kwenye kola­mu yangu hii kuwa hakuna mfanyabiashara ambaye anapenda kufanya kitu kwa hasara, hata kama ni tajiri mkubwa kiasi gani, hawezi kuwa anatoa tu fedha bila kuwa na mpangilio maalum wala bila kujua zitarudi vipi.

 

Alipokuwa akitoa misaada mingi ya kifedha nilijua ipo siku atataka irejee kwa njia anayoijua yeye, hata kama ilimchukua muda mrefu kuse­ma au kuweka wazi kile ali­chokuwa nacho kichwani laki­ni huo ndiyo ukweli kuwa Manji alikuwa na nia nzuri ya Yanga.

 

Siku zote unapokuwa kwenye vita kutokea kutofau­tiana na wenzako au kum­shambulia mwingine bahati mbaya ni mambo ya kawaida, Manji siyo malaika, alikuwa na makosa yake ya wazi na men­gine ambayo hatuyajui, lakini vita aliyopigwa ilikuwa nzito na yawezekana ilimzidi nguvu ndiyo maana akaishia njiani.

 

Wanayanga wengi walikuwa wanajisifu kwa timu yao kuto­kuwa na njaa na shida za fedha ndogondogo, hilo ni kweli lili­wezeshwa na Manji lakini wa­natakiwa kukubali kuwa fedha hizo zilikuwa zikitoka katika njia ambayo siyo sahihi, kama wanaosimamia soka wangea­mua kusimamia masuala ya matumizi ya fedha basi Yanga wangeingia kitanzini.

 

Katika soka kuna kitu kinait­wa ‘financial fair play’ yaani fedha za soka zitumike katika masuala ya soka, Yanga kwa asilimia kubwa chini ya Manji ilitumia fedha za mfukoni za bosi wao huyo na ndiyo maa­na walikuwa wababe, hivyo Manji alilijua hilo na ndiyo maana akasisitiza kuwa ni vema njia sahihi zikafuatwa.

 

Alitaka hilo kwa kuwa haku­taka kuende­lea kutoa fedha kiholela huku akitambua ipo siku itafika at­ageukwa na wale wataka­ohitaji mfumo sahihi wa kuion­goza klabu ili yeye aingize faida na klabu pia ipate faida, mwisho wake i k a s h i n d i k a ­na akaamua k u j i o n d o a .

K u j i o n d o a kwa Manji n i l i t e g e m e a sasa wale w a l i o k u w a w a k i m p i n g a kwa nguvu zote na ku­muona hafai basi wangeingia wao kwa kuwa wangekuwa wameshapata picha kuwa Manji anataka nini au ali­taka kuifanyia nini Yanga.

 

Matokeo yake, Yanga im­eendelea kuwa na hali ngu­mu, mara kadhaa wachezaji wameonyesha hilo kwa vi­tendo, lakini kukawa na siasa za hapa na pale kuonyesha kuwa kila kitu kiko sawa.

 

Yanga ni taasisi kubwa na katika dunia ya sasa un­apoona klabu kama hiyo inakuwa na nafasi ya ku­fika mbali kutoka na maliasili watu iliyonayo, kisha wache­zaji wakaendelea kulia njaa ni jambo baya kibiashara.

 

Najua kuna wapingaji wengi wa maendeleo kwa kuwa wa­najua klabu kama Yanga au Simba inapoendelea kuwa na maisha ya kuungaunga ndiyo wao wanavyoendesha maisha yao, kwa mwendo ilionao ni kitu kibaya sana kwa Yanga kuendelea kulia njaa huku mtaji watu upo.

Vuvuzela Mawasiliano na John Joseph  +255 713 393 542

Spoti Hausi: Said Maulid ‘SMG’ Ampa Mchongo Lwandamina

Leave A Reply