Taarifa zinaeleza kuwa kabla ya tukio, mtuhumiwa allikuwa akiishi na watoto wake watatu ambao mapacha hao aliwazaa na mama anaejulikana kwa jina la Deovitha David ambae kwa sasa wamekwisha achana na kubaki kama mzazi mwenzake.
Duru zinazidi kueleza kuwa marehemu hao mapacha kabla ya mauti kuwafika, mama yao alimuomba mzazi mwenzake kuja kuwachukua wanae wakamtembelee na kisha atawarejesha, mtuhumiwa alimkubalia mzazi mwenzake na kumtaka awarejeshe watoto hao Jumamosi ya tarehe 15 April, na baada ya mapacha hao kuwa wamerejeshwa, mama huyo aliondoka zake ambapo tukio la la mauaji hayo lilifanyika usiku huo wakati mama huyo akiwa tayari amekwisha rejea katika mji wake.
Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo ambae pia ni mtoto mdogo wa kumzaa, Japhet Respicius (5) alisema usiku wa tukio baba yake mzazi aliwachukua marehemu hao kwa zamu na kisha kutelekeza mauaji hayo, na alipojaribu kuhoji walipo ndugu zake alimjibu kuwa wapo mbinguni.
Mtoto ndiye alikuwa wa kwanza kutoa taarifa kwa ndugu jamaa na majirani ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa kijiji Bulambuzi.
Kisa kamili cha mauaji hayo mpaka sasa hakijajulikana japo inahusishwa na mgogoro wa kimapenzi uliokuwa ukiendelea kati ya wanandoa haona wengine wakihusisha na kile walichokiita wivu wa mapenzi. Juhudi za kutaka kuhahamu ukweli kutoka mama wa marehemu zimeshindikana mpaka sasa kutokana na majonzi na huzuni mkubwa uliopelekea mama huyo kushindwa kabisa kuongea na vyombo vya habari.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema baada ya msako mkali, mtuhumiwa ametiwa mbaroni jana Aprili 16 jijini Mwanza baada ya kutoroka na taratibu za kumsafirisha ili akabiliane na mashitaka zinafanyika.
UNYAMA WA KUTISHA! Baba Achinja Wanaye Mapacha, Mtoto Asimulia!
MAFURIKO DAR
Comments are closed.