Taasisi za Serikali, Dini na Kiraia Zatakiwa Kufuata Maadili
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Suzan Mlawi, akizungumza jambo kwenye hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Ayoub Rioba (kushoto) akichangia mada katika hafla hiyo.
Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, akihojiwa na wanahabari kuhusiana na mdahalo huo.
Suzan Mlawi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mdahalo huo.
Na Denis Mtima/GPL
NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Suzan Mlawi, amezitaka taasisi za serikali, dini na asasi za kiraia kufuata maadili yanayotakiwa katika kazi zao.
Hayo ameyasema leo wakati akizindua mdahalo wa asasi hizo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam uliojadili mada mbalimbali hasa zilizokuwa zikilenga masuala ya maadili na haki za binadamu kuelekea maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu yanayotarajiwa kufanyika hivi karibuni.
Comments are closed.