The House of Favourite Newspapers

Waziri Mbalawa Azindua Huduma ya Kuhama Mtandao

Waziri wa Ujenzi Uchukuaji na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akizungumza katika hafla hiyo.

DAR ES SAALAM: Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) jana imezindua rasmi huduma ya mawasiliano ya simu ya kuhama mtandao mmoja kwenda mwingine bila kubadilisha namba ya awali. (Mobile Number Portability ‘MNP’).

Meza kuu Ilivyoonekana kutoka kulia ni James Kilaba, Waziri Mbalawa na Jonis Kimbe

Akizungumza katika hafla hiyo, iliyofanyika Makao Makuu ya Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kilaba mbele ya Waziri wa  Ujenzi Uchukuaji na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ambaye alikuwa mgeni rasmi, aliyataja mambo hayo 10 ya kuzingatia kwa mtumiaji:

 

Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla hiyo.

GHARAMA YA LAINI

Kampuni ya simu husika inahitajika kumpa mteja laini mpya aidha bure au kukmuuzia bila gharama zingine zaidi.

Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla hiyo.

KUSHAWISHIWA

Mtoa huduma wa awali haruhusiwi kumshawishi mteja kubaki kwenye huduma yake kwa namna yoyote ile, akifanya hivyo mteja anapaswa kutoa taarifa  TCRA, ila anaweza kuahirisha kuhama mwenyewe, kabla hajatuma ujumbe wa HAMNA KWENDA 15080.

MTEJA MPYA

Kwa mteja mpya aliyesajiliwa na kampuni husika hivi karibuni, anaruhusiwa kuhamia mtandao mwingine baada ya siku 60.

KUJUA NAMBA ULIYOHAMA

Mteja akipiga simu kwenye namba aliyohama, atagundua imehamia mtandao mwingine kwa kusikia sauti ya milio miwili mifupi (beeps) unapoanza tu kupiga. Mlio huo utamtaarifu gharama za simu unayopiga inaweza kuongezeka zaidi.

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kilaba akizungumza jambo katika hafla hiyo.

KUTUMA FEDHA NAMBA ILIYOHAMA

Mteja anapotuma fedha kwenda namba aliyohama, atapewa taarifa ili awe na maamuzi ya kutuma au la! Kulingana na taratibu za mtandao husika.

 

MUDA WA KUPATIKANA HUDUMA

Huduma hiyo imeanza kutolewa rasmi leo (Machi Mosi, 2017), maduka, ofisi na maeneo ya mauzo ya mtoa huduma wako mpya wanaendelea na huduma kawaida.

 

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano TCRA naye akizungumza jambo.

KUHUSU SIMU BENKI

Kutokana na mteja anayehamia mtandao mwingine kupewa namba mpya, hivyo anapaswa kuwasiliana na tawi la benki yake ingawa inategemeana na benki kama inatoa huduma ya simu benki.

 

MUDA WA MAONGEZI

Mteja aliye na salio la muda wa maongezi, anapaswa kutumia salio lake lote kabla ya kuhama vinginevyo salio linaweza kupotea.

 

FEDHA MTANDAO

Kwa mteja mwenye salio la pesa kwenye simu yake anapaswa atoe kwanza pesa yake kabla hajahama, vinginevyo itabidi afuate taratibu zingine kupata pesa yake. Ila muda wote pesa itakuwa salama.

 

…halfa hiyo ikiendelea.

Uzinduzi rasmi wa kuhama mtandao mmoja kwenda mwingine ukifanyika kwa Kubofya kwende kumpyuta mpakato.

MALALAMIKO AU MAOMBI

Kwanza wasiliana na mtoa huduma wako mpya ili kupata ufumbuzi, usiporidhika toa malalamiko yako TCRA.

Comments are closed.