UVCCM: Wahandisi Zanzibar Jengeni Barabara Bora
UVCCM imesema kuwa serikali inapaswa kuwachukulia hatua za kisheria wahandisi hao ikiwemo kuwanyima tenda sambamba na kuwafikisha mahakani kwani wanaisababishia hasara kubwa serikali kwa kufanya marekebisho ya barabara mara kwa mara.
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka Hamdu Shaka leo alipokuwa akikagua ujenzi wa barabara ya OleVitongoji na Mfukiwa-Kengei wakati wa ziara ya kikazi ya ukaguzi wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Wilayani Chakechake Mkoa wa Kusini Unguja.
Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 35 inatarajiwa kukamilika katika hatua za awali mwishoni mwa mwezi Agosti mwaka huu huku ukamilisho wote ukitarajwai kufika ukomo Desemba mwaka kesho.
Shaka amepongeza namna barabara hiyo inavyojengwa kwa viwango ambayo itakuwa na uwezo wa kudumu kwa muda mrefu pasina kufanyiwa marekebisho ya mara kwa mara kama ambavyo baadhi ya barabara zimekuwa zikiharibika na kufanyiwa marekebisho jambo ambalo linaiingizia serikali hasara.
Hadi kufika hatua ya ukamilisho barabara hiyo itagharimu Dola za Marekani milioni 11 ambazo ni sawa na zaidi ya Shilingi Bilioni 24.4
Barabara hiyo inajengwa na Wizara ya Ujenzi na Utunzaji wa Barabara Zanzibar upande wa Pemba kupitia ufadhili wa mfuko wa nchi zinazotoa mafuta kwa wingi duniani (OPEC).
Naye Meneja Mradi wa barabara hiyo Mhandisi Amin Halid Abdallah amempongeza Shaka kwa kuzuru eneo hilo kujionea hali ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM huku akiahidi kusimamia ujenzi huo kwa weledi na hatimaye kuwa na barabara imara.