The House of Favourite Newspapers

Koletha: Ndoa Kudumu Ni Mungu Tu

Staa wa Koletha Raymond.

MKONGWE wa filamu za Kibongo, Koletha Raymond amefunguka kuwa suala la kudumu kwenye ndoa ni la Mungu tu kwani kwa akili zake hawezi kujihakikishia kwa asilimia mia moja.

 

Koletha alisema hayo kutokana na ndoa nyingi za mastaa kutodumu ambapo alisema ingawa ana imani ndoa yake itadumu, lakini ni Mungu pekee ndiye mwenye uwezo wa kulijua hilo kwa ufasaha.

 

“Kikubwa ni kumshirikisha Mungu tu kwa kweli na mimi mwenyewe kuchezea karata yangu vizuri, siwezi kusema ndoa yangu itadumu milele, ni kwa neema tu maana kuna mengine hayavumiliki,” alisema Koletha.

Stori: Gladness Mallya | Risasi Jumatano

Comments are closed.