Ray C Aibuka Na Mahaba Kimbunga Kutoka Tornado
MWANAMUZIKI maarufu nchini Tanzania Rehema Chalamila ‘Ray C’, baada ya ukimya wa muda mrefu hatimaye ameibuka upya na wimbo mpya unaokwenda kwa jina la TORNADO jina lenye maana ya kimbunga cha mahaba.
Ray C anaibuka katika wimbo huo akiwa ameshirikishwa na msanii kutoka nchini Kenya Dennis Mwangi aka Papa Dennis mwenye makazi yake nchini Kenya ambapo yupo chini ya labo ya Maliza, wimbo huo tayari upo katika video ambayo imetengenezwa nchini Afrika ya Kusini na muongazaji wa video maarufu Afrika, God Father.
Mbali na wimbo huo Papa Dennis ameshafanya nyimbo na vinara wengi wa muziki wa Afrika akiwemo Mr Flavour (Nigeria) ,Chiddimna (Nigeria) ,Korode bello (Nigeria) na sasa Ray – C (Tanzania)
Comments are closed.