The House of Favourite Newspapers

UFARANSA YAANZA VIZURI KOMBE LA DUNIA DHIDI YA AUSTRALIA

Ufaransa imefanikiwa kuibuka na ushindi wake wa kwanza katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu nchini Russia wa mabao 2-1 dhidi ya Australia.

 

Mabao ya mchezo huo yametiwa kimiani na Antoine Griezmann katika dakika ya 58 kwa njia ya mkwaju wa penati na la pili likitiwa kimiani na Paul Pogba (80′).

Bao pekee la Australia liliwekwa wavuni na Mile Jedinak mnamo dakika ya 62 kwa mkwaju wa penati.

Mechi hii imekuwa ya kwanza kushuhudiwa penati mbili ndani ya dakika 90 zikipigwa kwa pande zote.

 

Ushindi huu wa Ufaransa unawapa alama tatu muhimu kwenye kundi C ambapo baadaye Peru na Denmark watakuwa wanacheza pia kutoka kundi hilo.

FRANCE (4-3-3): Lloris; Pavard, Varane, Umtiti, Lucas; Tolisso (Matuidi 77), Kante, Pogba; Dembele (Fekir 69), Mbappe, Griezmann (Giroud 69)

Subs not used: Mandanda, Kimpembe, Lemar, Nzonzi, Rami, Sidibe, Thauvin, Mendy, Areola

Goals: Griezmann 58 (pen); Pogba 80

Booked: Tolisso

AUSTRALIA (4-4-1-1): Ryan; Risdon, Milligan, Sainsbury, Behich; Leckie, Jedinak, Rogic (Irvine 71), Mooy; Kruse (Arzani 83); Nabbout (Juric 64)

Subs not used: Jones, Degenek, Meredith, Cahill, Jurman, Luongo, Maclaren, Petratos, Vukovic

Goal: Jedinak 62 (pen)

Booked: Leckie, Risdon, Behich

Referee: Andres Cunha (Uruguay)

Comments are closed.