Luke Shaw Anakula ‘Bata La Kufa Mtu’
BEKI wa kushoto wa Manchester United, Luke Shaw ameweka shida chini na kuamua kurusha mikono juu kisha ‘kubanjuka tu’.
Shaw ambaye alikuwa katika wakati mgumu msimu uliopita chini ya Kocha Jose Mourinho kutokana na kukosa namba kikosi cha kwanza ameonekana kuwa mbali na maisha ya soka baada ya kutumia muda mwingi akila raha.
Beki huyo mwenye umri wa miaka 22 ambaye pia ametoswa kwenye timu ya taifa ya England, ameonekana akiwa kwenye boti binafsi akila raha na rafiki zake huku wad a d a wakiwa wengi wakimzungua.
Msimu uliopita alicheza mechi 11 za Premier League baada ya kuwa chaguo la pili nyuma ya mkongwe Ashley Young.
Comments are closed.